Mnamo Jumatatu tarehe 21 Agosti, tukio lisilo la kawaida litashuhudiwa Amerika Kaskazini, ambalo limewavutia watu zaidi ya milioni saba wanaotarajia kulishuhudia katika miji mbalimbali Marekani.
Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani.
Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana, Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa.
Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia.
Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa.
Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri sana kwa hamu majira haya ya joto.
Kuna watu 12 milioni ambao wanaishi eneo la upana wa maili 70 9kilomita 112) kutoka Oregon hadi Carolina Kusini ambapo mwezi utalifunika kabisa jua.
Utalii wa "kutazama kupatwa kwa jua" unatarajiwa kuwazolea pesa nyingi sana, utalii ambao ulianza kupata umaarufu karne ya 18 ambapo watu wengi walisafiri hadi miji ambayo jua lingepatwa na mwezi Ulaya.
Lakini ni kwa nini tukio hili nadra sana linavutia watu wengi na pia kwa wengine kuibua wasiwasi?
Wasiwasi zama za kale
Katika karne ya 7 kabla ya kuzaliwa kwa yesu Kristo, mshairi maarufu Archilocus aliandika kuhusu kutokea kwa tukio hilo katika ksiiwa cha Paros, Ugiriki: " Hakuna jambo linaloweza kunishangaza tena duniani sasa. Kwani Zeus, babake Olympian, amegeuza mchana kuwa usiku wa giza kwa kulifunika jua, na sasa ukatili wa giza unawakodolea macho binadamu. Jambo lolote linaweza kutokea."
Watu wengi hawakufahamu kabisa nini kilitokea wakati wa jua kupatwa na mwezi, hadi karne ya 17, anasema Edwin Krupp, mkurugenzi wa kituo cha kutafiti anga za juu cha Griffith jimbo la California.
Wagiriki hawakuwa peke yao katika kuingiwa na wasiwasi.
Ingawa kuna wasomi kadha kuanzia karne ya 8 tangu kuzaliwa kwa Yesu ambao walianza kufahamu jua hupatwa vipi na mwezi, kwa miaka mingine 2,000, watu wengi duniani walihusisha tukio hilo na miungu.
Krupp anasema kwa muda mrefu, watu walijaribu kufafanua yaliyokuwa yakitokea na mambo na vitu vilivyowazunguka.
Hadi wa leo, baadhi ya maeneo duniani bado kuna itikadi kuhusu tukio la mwezi jua kupatwa na mwezi.
Nchini India, kuna baadhi ya wajawazito hawawezi kutoka nje ya nyumba zao wakati wa tukio hilo kwa sababu wanaogopa wanaweza kupatwa na madhara.
Ili kukabiliana na wasiwasi huo, baadhi ya jamii zilianza kufanya matambiko, wakijaribu kuwasiliana na nguvu au mashetani ambao waliamini walihusika katika kuliziba jua.
Kwa mara ya kwanza tangu 1918, jua litapatwa kikamilifu na mwezi Marekani.
Bara lote la Amerika Kaskazini litafunikwa na giza totoro mchana, Ingawa baadhi ya watu wanalitazama tu kama tukio la kuvutia, kwa wengine, hili linaashiria mwisho wa dunia kama tunavyoifahamu kwa sasa.
Makundi mbalimbali ya Kiinjilisti nchini Marekani kwa mfano, yameanza kuhubiri kwamba tukio hilo linaashiria kukaribia kwa mwisho wa dunia.
Tovuti moja ya unabii wa Kikristo kwa jina Unsealed imedai kwamba tukio hilo la Jumatatu litaanzisha kipindi cha Majonzi, kipindi cha miaka saba ambapo katika kipindi hicho asilimia 75 ya watu wote duniani wataangamizwa.
Kwa wengine hata hivyo, ni tukio ambalo wamesubiri sana kwa hamu majira haya ya joto.
Kuna watu 12 milioni ambao wanaishi eneo la upana wa maili 70 9kilomita 112) kutoka Oregon hadi Carolina Kusini ambapo mwezi utalifunika kabisa jua.
Utalii wa "kutazama kupatwa kwa jua" unatarajiwa kuwazolea pesa nyingi sana, utalii ambao ulianza kupata umaarufu karne ya 18 ambapo watu wengi walisafiri hadi miji ambayo jua lingepatwa na mwezi Ulaya.
Lakini ni kwa nini tukio hili nadra sana linavutia watu wengi na pia kwa wengine kuibua wasiwasi?
Wasiwasi zama za kale
Katika karne ya 7 kabla ya kuzaliwa kwa yesu Kristo, mshairi maarufu Archilocus aliandika kuhusu kutokea kwa tukio hilo katika ksiiwa cha Paros, Ugiriki: " Hakuna jambo linaloweza kunishangaza tena duniani sasa. Kwani Zeus, babake Olympian, amegeuza mchana kuwa usiku wa giza kwa kulifunika jua, na sasa ukatili wa giza unawakodolea macho binadamu. Jambo lolote linaweza kutokea."
Watu wengi hawakufahamu kabisa nini kilitokea wakati wa jua kupatwa na mwezi, hadi karne ya 17, anasema Edwin Krupp, mkurugenzi wa kituo cha kutafiti anga za juu cha Griffith jimbo la California.
Wagiriki hawakuwa peke yao katika kuingiwa na wasiwasi.
Ingawa kuna wasomi kadha kuanzia karne ya 8 tangu kuzaliwa kwa Yesu ambao walianza kufahamu jua hupatwa vipi na mwezi, kwa miaka mingine 2,000, watu wengi duniani walihusisha tukio hilo na miungu.
Krupp anasema kwa muda mrefu, watu walijaribu kufafanua yaliyokuwa yakitokea na mambo na vitu vilivyowazunguka.
Hadi wa leo, baadhi ya maeneo duniani bado kuna itikadi kuhusu tukio la mwezi jua kupatwa na mwezi.
Nchini India, kuna baadhi ya wajawazito hawawezi kutoka nje ya nyumba zao wakati wa tukio hilo kwa sababu wanaogopa wanaweza kupatwa na madhara.
Ili kukabiliana na wasiwasi huo, baadhi ya jamii zilianza kufanya matambiko, wakijaribu kuwasiliana na nguvu au mashetani ambao waliamini walihusika katika kuliziba jua.

Comments
Post a Comment